• RSS
  • Email
  • Follow us
  • Become a fan
  • TOp cat Nav1
  • TOp cat Nav1
  • Top cat Nav1

SpicyTricks

  • Cat Nav
    • Sub cat Nav1
    • Sub Cat Nav2
  • cat Nav
  • cat Nav
  • cat Nav

TRA KUDHIBITI KAZI ZA WASANII

Na Ferdinand Shayo,Arusha.
Mamlaka ya Mapato nchini imeanzisha mfumo wa kutoa stempu kwa kazi za wasanii ili kudhibiti unyonywaji wa kazi  hizo unaofanywa na baadhi ya wasambazaji na wazalishaji feki hivyo kuwafanya wasanii wanufaike na kazi zao pamoja na kulipa kodi kwa serikali.

Akizungumza na Wasanii wa muziki na filamu jijini Arusha ,Afisa elimu kwa mlipakodi TRA,Frank Mwaselela amesema kuwa mfumo huo tayari umerasimishwa kisheria na baada ya kutoa elimu kwa wasambazaji na wasanii hakuna kazi yeyote itakayoruhusiwa kuuzwa pasipo kuwa na stempu.

Afisa huyo amesema kuwa mfumo huo utawasaidia wasanii kutoibiwa kazi zao  na pia kazi zao kuwa na ulinzio wa kisheria baada ya kupitia taratibu sahihi ambazo ni kuzisajili baraza la sanaa (BASATA) Na pia kwa baraza linalohusika na haki miliki (COSOTA).

Naye Afisa  Kodi  Msafiri Mbibo kutoka makao makuu ya TRA amesema kuwa mfumo huo wa stempu umeanza mwaka jana   utasaidia kuondoa wimbi kubwa la wizi na uharibifu wa kazi za sanaa .
“Mpango huu utasaidia kuhakikisha kuwa wasanii kuwa mikataba inayozingatia  haki za wasanii,tayari tuimeshaanza kufanya operesheni kuwakamata wanaouza kazi zisizo na stempu na kuharibu mashione mkoa wa Dar tutaelekea mikoani pia” Alisema Afisa huyo


Katibu wa Chama cha Wauzaji wa kazi za wasanii jijini hapa James Male amesema kuwa jitahada zinazofanywa na TRA na Serikali ni nzuri na ameiomba mamlaka hiyo kuzitazama kazi walizonunua miaka ya nyuma kabla ya kuanzishwa kwa mfumo wa stempu.
Mwenyekiti wa Chama cha Wasanii mkoani Arusha ,Kassim Digega ameipongeza mamlaka hiyo kwa kuonyesha nia ya dhati ya kulinda kazi zao ili waweze kunufaika na kulinufaisha taifa kwa kulipa kodi.

VITAMBULISHO VYA TAIFA KUWAFIKIA LINDI NA MTWARA

Mkurugenzi wa Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa (NIDA) , Dickson Maimu amesema kuwa zoezi la usajili wa watu na kuwapatia vitambulisho  hivyo litaanza katika mikoa ya Lindi,Mtwara na Pwani  hivi karibuni hivyo amewataka wananchi kutoa ushirikiano ili kufanikisha zoezi hilo.


Aidha Mkurugenzi huyo amesema kuwa baada ya kukamilisha zoezi hilo katika mikoa ya Dar es Salaam na mikoa yote mitano ya Zanzibar sasa wanaelekea katika mikoa hiyo .

Akizungumza katika mkutano wa Wafanyakazi wa  Mamlaka hiyo unaoendelea jijini hapa amesema kuwa vitambulisho hivyo vitawasaidia Watanzania kukopesheka kwa urahisi baada ya kutambulika hivyo kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja na taifa kwa Ujumla,pia kuwatambua wageni na wakimbizi.
Maimu amesema kuwa serikali imetenga fedha za kutosha katika bajeti kiasi cha shilingi bilioni  200 ambazo zitasaidia kufanikisha zoezi hilo na kulikamilisha,tunatarajia baada  ya mikoa hiyo itafuata Kilimanjaro,Arusha na Tanga.
 
Mkurugenzi wa Mamlaka ya vitambulisho vya Taifa (NIDA) , Dickson Maimu akiwa anaongea na waadhishi wa habari kuhusiana na zoezi lima la ugawaji wa kitambulisho cha taifa




Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Arusha ,Nyirembe Munasa amesema kuwa licha ya vitambulisho hivyo kuwasaidia wananchi kiuchumi vitawasaidia katika masuala ya ulinzi na usalama ,kutatusaidia kuwatambua wachafuzi wa amani inawezekana wanatoka nje pia kudhibiti ugaidi.
Nyirembe ameitaka Mamlaka hiyo kuhakikisha kuwa inatoa elimu ya kutosha kwa wananchi kwa kupitia vyombo vya habari na taasisi mbali mbali zikiwemo shule na vyuo ili watanzania wajue umuhimu wa vitambulisho hivyo .

Naye Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo kwa upande wa Zanzibar,Vuai Suleman alisema kuwa tayari zoezi hilo limekamilika katika nchi hiyo yenye mikoa 5 na wilaya 10.amewataka watanzania kutoa ushirikiano na kuwa na taarifa muhimu ikiwemo kitambulisho cha mkazi,cheti cha kuzaliwa,vyeti vya kukupigia kura ili kufanikisha zoezi hilo la kitaifa.
Newer Posts Home
  • Recent Posts
  • Feature Posts
  • Comments

Archive

  • 2014 (2)

Catwidget1

Catwidget2

Catwidget3

Catwidget4

AFRICA ONESTORY © 2011. All rights reserved. Designed by Gadiola Emanuel